Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akiangalia makopo yanayotumiwa na Kiwanda cha Kamal kama nalighafi za kiwanda akiwa na uongozi wa kiwanda.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akimuangalia fundi wa kusawazisha chuma kwa kutumia Shaper Mashine.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
WAZIRI wa viwanda,biashara na uwekezaji, Charles Mwijage amelitaka shirika la viwango hapa nchini (TBS) kuhakikisha wale wote wanaotaka kuingiza vilainishi mitambo kutoka nje ya nchi wanatoa taarifa kabla ya tarehe 1 mwezi wa 5 mwaka huu ili kupambana na bidhaa bandia.
Mwijage ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika viwanda vitatu vya vilainishi mafuta na kiwanda kimoja cha nondo vilivyopo manispaa ya temeke jijini Dar es Salaam ambapo ameeleza kuwa ziara hyo imelenga kuhakikisha watanzania wanapata bidhaa bora na zinazokidhi mahitaji ya watumiaji wa bidhaa hizo.
Aidha Mwijage amewaagiza waendeshaji wa viwanda hivyo kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora kwani vilainishi mitambo vina umuhimu mkubwa sana hasa kudhibiti ajari mbalimbali katika mitambo ya uendeshaji shughuli za kimaendeleo.
Katika ziara hiyo mh. Mwijage alianza katika kiwanda cha nondo cha kamal steel, akaenda kiwanda cha vilainishi mitambo cha fuchs pia alienda katika kiwanda cha vilainishi mitambo cha general petroleum na kumalizia ziara yake katika kiwanda cha kuzalishilia vilainishi vya mitambo cha oryx vyote vikiwa manispaa ya temeke jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
WAZIRI wa viwanda,biashara na uwekezaji, Charles Mwijage amelitaka shirika la viwango hapa nchini (TBS) kuhakikisha wale wote wanaotaka kuingiza vilainishi mitambo kutoka nje ya nchi wanatoa taarifa kabla ya tarehe 1 mwezi wa 5 mwaka huu ili kupambana na bidhaa bandia.
Mwijage ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika viwanda vitatu vya vilainishi mafuta na kiwanda kimoja cha nondo vilivyopo manispaa ya temeke jijini Dar es Salaam ambapo ameeleza kuwa ziara hyo imelenga kuhakikisha watanzania wanapata bidhaa bora na zinazokidhi mahitaji ya watumiaji wa bidhaa hizo.
Aidha Mwijage amewaagiza waendeshaji wa viwanda hivyo kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora kwani vilainishi mitambo vina umuhimu mkubwa sana hasa kudhibiti ajari mbalimbali katika mitambo ya uendeshaji shughuli za kimaendeleo.
Katika ziara hiyo mh. Mwijage alianza katika kiwanda cha nondo cha kamal steel, akaenda kiwanda cha vilainishi mitambo cha fuchs pia alienda katika kiwanda cha vilainishi mitambo cha general petroleum na kumalizia ziara yake katika kiwanda cha kuzalishilia vilainishi vya mitambo cha oryx vyote vikiwa manispaa ya temeke jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...