Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (kushoto) akiwa pamoja na wanamuziki wa kundi la Navy Kenzo Nahreel na Aika (katikati) pamoja na Meneja Msoko wa Airtel Bi Anethy Muga wakionyesha bango la Uzinduzi wa huduma mpya ya kifurushi kipya cha Airtel Yatosha kijuikanacho kama “Jipimie Yatosha yako” kitakachowawezesha wateja kutengeneza na kununua kifurushi wanachokitaka kutokana na chaguo na mahitaji yao
Meneja Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando (wa pili kulia) akiongea na waandishi wa habari wakati wa Uzinduzi wa huduma kifurushi kipya cha Airtel Yatosha kijuikanacho kama “Jipimie Yatosha yako” kitakachowawezesha wateja kutengeneza na kununua kifurushi wanachokitaka kutokana na chaguo na mahitaji yao. Kushoto ni Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga na wakwanza toka kulia ni wanamuziki wa kundi la Navy Kenzo Nahreel akifatiwa na Aika
Meneja Msoko wa Airtel Bi Anethy Muga (kulia) kiongea wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijuikanacho kama “Jipimie Yatosha yako” kitakachowawezesha wateja kutengeneza na kununua kifurushi cha wanachokitaka kutokana na chagua na mahitaji yao. Pichani ni Meneja Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando pamoja na wanamuziki wa kundi la Navy Kenzo Nahreel akifatiwa na Aika
Wanamuziki wa kundi la Navy Kenzo Nahreel na Aika wakijaribu kujipimia kifurushi cha Airtel Yatosha mara baada ya kuzindua huduma hiyo mpya leo, wpamoja nao ni Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando (shoto). “Jipimie Yatosha yako” itawawezesha wateja kutengeneza na kununua kifurushi wanachokitaka kutokana na chaguo au mahitaji yao.
· Kwa mara ya kwanza Tanzania unajipimia vifurushi vya Airtel Yatosha UTAKAVYO
· Jiunge na Airtel ufurahie uhuru wa kujitengenezea kifurushi chako mwenyewe kwa gharama nafuu
Dar es salaam Aprili 11, 2016, Airtel Tanzania ili kutoa uhuru zaidi kwa wateja wake imetangaza kifurushi kipya kupitia huduma yake ya vifurushi vya Airtel Yatosha kijulikanancho kama Airtel Jipimie Yatosha Yako itakayowapa wateja wake faida kubwa na uwezo wa kuweza kupanga na kuunda kifurushi wanachokitaka kutokana na chaguo na mahitaji yake .
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Airtel Bi, Anethy Muga alisema "Jiunge sasa na Airtel ufurahie Uhuru huu mpya, Tumezindua " Airtel Jipimie Yatosha Yako " kwa ajili ya kuwapatia wateja wetu uhuru wa kuchagua na kupanga matumizi yao na papo hapo kuunda kifurushi kitakachoweza kukidhi mahitaji yao ya kiuchumi na kijamii.
Airtel Jipimie Yatosha Yako "ni moja ya kifurushi cha kibunifu zaidi ambacho na kinapatikana kwa wateja wetu wote hapa nchini ambapo unaweza kupata kifurushi hiki upendavyo wewe yaani kwa siku, wiki, na hata mwezi.
“Airte daima tunafanyia bidhaa zetu zote utafiti na kuziunda kwa mujibu wa kile wateja wetu wanataka ili kuleta unafuu na ubora zaidi, kwa mara ya kwanza nchini Tanzania wateja wa simu za mkononi wa Airtel wataweza kuamua kununua vifurushi vya gharama nafuu na watakavyo vya hadi shilingi 500 huku wakijipimia muda wa maongezi tu, au changanya na MB zaidi au unajichaguali Muda wa maongezi na SMS au kujipimia vyote yaani Muda wa maongezi Zaidi, MB zaidi na SMS Zaidi, uhuru ni wako kujipimia utakavyo” na sasa ndio wakati wa kujiunga na Airte.
Airtel inaamini ubunifu wa huduma ya “Jipimie Yatosha Yako" itakuwa suluhisho la mawasiliano kwa wengi na msaada kwa wale ambao walitaka kifurushi kutokana na hitaji lake. Sasa wateja wa Airtel wanauwezo wa kutengeneza Yatosha yao wao wenyewe na kutimiza mahitaji yao .
Kujiunga na kifurushi cha Yatosha na kufurahia Jipimie Yatosha Yako, wateja wanatakiwa kupiga namba *149*99# na kuchagua namba 5 ‘Jipimie Yatosha Yako’ na kutengeneza kifurushi cha chaguo lake.
Huduma mpya ya uhuru wa kujipimia Vifurushi vya Yatosha imezinduliwa na kusindikizwa na wasanii wa kundi la Navy kenzo linaloundwa na Nahreel na Haika ambao wataitambulisha sehemu mbalimbali nchini.“Sisi tuko tayari kama kawaida kuja kujipimia yatosha kila mahali, sasa na nyie kuweni tayari kukamatia chini Yatosha yako inayokutosha" alisema Nahreel wa Navy Kenzo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...