Msanii wa bongo fleva Saraha ambaye ni raia wa Sweden ametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden jijini Stockholm leo na kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi Dora Msechu.
Saraha hivi sasa anatamba kwenye anga za muziki nchini Sweden na nyimbo  ya "Kizunguzungu" ambayo ameimba kwa lugha ya kiswahili.
Balozi Dora Msechu amempongeza Saraha kwa mafanikio makubwa aliyopata kwa wimbo huo ikiwa ni pamoja na  kuingia fainali ya mashindano makubwa ya kutafuta nyimbo bora hapa Sweden, Melodifestivalen. 
Mhe. Balozi amemshukuru sana Saraha kwa kuitangaza vyema Tanzania na kusambaza lugha ya kiswahili  nchini Sweden kupitia fani ya muziki.
Kwa upande wake, Saraha ameeleza kuwa amepata faraja kubwa sana kukaribishwa na Mhe. Balozi  kutembelea Ubalozi wa Tanzania na amefurahi sana kupata fursa ya kuzungumza Kiswahili. 
Saraha amesema  kuwa ana mapenzi makubwa sana na Tanzania  na ataendelea kutumia lugha ya kiswahili katika kazi zake za usanii hapa Sweden. Amebainisha kuwa  hivi sasa yupo mbioni kutoa nyimbo nyingine kali ya kiswahili hapa Sweden.
Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Dorah Msechu akiongea na mwanamuziki Saraha na meneja wake walipotembelea ubalozini jijini Stockholm leo.
Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Dorah Msechu akipozi na mwanamuziki Saraha alipotembelea ubalozini jijini Stockholm
Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Dorah Msechu na watumishi wa ubalozi wakipozi na mwanamuziki Saraha alipotembelea ubalozini jijini Stockholm. Cheki video yake ya ngoma yake kali ya  "Kizunguzungu" hapa chini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huyu ni dada yake mzunvu kichaa? Naona atamshinda Diamond kabisa. Nice song!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...