Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob akizungumzana wa wafanyabiashara ndogo ndogo waeneo la Ubungo Stendi ya Mkoa kuhama katika eneo hilo na kuhamia katika kituo cha mabasi Simu 2000, leo jijini Dar es Salaam.
Wafanyabiashara ndogo ndogo waeneo la Ubungo Stendi ya Mkoa wakijibapanga kwenye maeneo yao waliypewa bure na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob leo jijini Dar es Salaam.
Wafanyabiashara ndogo ndogo waeneo la Ubungo Stendi ya Mkoa wakimsikiliza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).

Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Boniface Jacob leo amefanya ziara katika eneo la ubungo na kuongea na wafanyabiashara ikiwemo kuwaonyesha eneo la kufanya biashara zao.

Amewataka wafanyabiashara hao kesho wasiwepo maeneo hayo na kuwataka kuhamishia biashara zao katika eneo la soko la Mawasiliano (Sinza), kwani wasipofanya hivyo Kamati ya Ulinzi na Usalama Manispaa ya Kinondoni imeshakaa na imepanga kuwaondoa.

Meya alieleza kuwa isingekuwa busara kuwaondoa bila kuwaeleza watakwenda wapi, Meya amewakabidhi wafanyabiashara hao kadi ambazo watazionyesha ili wasisumbuliwe,pia amewataka wasilipe pesa yeyote endapo watatakiwa walipie maeneo ya biashara waliyopewa.

Pia amesema kuhusu ushuru hawatalipa kwa muda wa mwezi mmoja baada ya hapo watalipia,Meya huyo amewahakikishia wafanyabiashara hao kuwa hakuna atakayekosa eneo la kufanya biashara.

Afisa biashara wa Manispaa ya Kinondoni amewataka wafanyabiashara hao kutokaidi agizo hilo la Meya,hivyo kuanzia kesho wataondolewa kwa nguvu.

Meya amesema kuna maeneo wamepewa madiwani akiwemo yeye na hayafanyiwi biashara, hivyo sio sawa maeneo hayo wapewe wafanyabiashara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...