Muogeleaji nyota wa kiume wa Tanzania, Hilal Hilal (wa kwanza kulia) akiwa kwenye jukwaa mara baada ya kupokea medali yake ya Shaba katika mashindano ya Kanda ya Nne ya Cana.
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kinanchoshiriki katika mashindano ya Cana Kanda ya nne. kutoka kulia ni Amani Doggart, Catherine Mason, Hilal Hilal na Smriti Gokarn.
Na Mwandishi wetu
Muogeleaji wa Tanzania, Hilal Hilal ametwaa medali ya Shaba katika mashindano ya kuogea ya Cana Kanda ya Nne yanayoendelea nchini Mauritius.
Hilal ambaye ni nahodha wa timu ya Taifa katika mchezo huo, amemaliza katika nafasi ya tatu katika staili ya butterfly kwa kutumia muda wa sekunde 26.70 katika mashindano hayo magumu yaliyoshirikisha nchi za Uganda, Kenya, Rwanda Burundi, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Somalia, Sudani Kusini na Sudan.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...