Naibu Katibu Mkuu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba (kushoto), Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo, Amani Mashaka (katikati), anayefuata ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Jenita Ndone wakiwaongoza wajumbe wa Baraza hilo kuimba wimbo wa mshikamano daima kabla ya Naibu Katibu Mkuu kufungua kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kabla ya kufungua mkutano wa siku moja wa baraza hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Jeshi la Magereza, Ukonga, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake Balozi Simba aliwataka watumishi wa wizara yake wafanye kazi kwa bidii ili kuiletea maendeleo wizara hiyo.
 Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Jeshi la Polisi, Arcado Nchinga akichangia mada katika kikao cha Baraza hilo kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza kwa makini Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan Simba (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe hao katika Mkutano wa Baraza hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam. 
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...