Katibu Shirikisho Vyuo Vya Elimu ya Juu Siraji Madebe
akizungumza leo na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam |
NA BASHIR NKOROMO.
Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya Juu CCM, limepongeza Uteuzi wa vijana, Salum Happi na Humphrey Polepole kuwa wakuu wa wilaya uliofanywa hivi karibuni.
Katika pongezi hizo, Katibu wa Shirikisho hilo, Siraji Madebe, amewataka Happi (Kinondoni) na Polepole (Musoma) na Vijana wengine waliopatiwa nafasi mbalimbali, kuchapa kazi kwa bidii ili wasi kuendelea kuudhihirishia umma wa Watanzania kwamba Vijana wanao uwezo wa kushika madaraka.
Amesema, ni muhimu wajitume kwa sababu kutochapa kazi kwa bidii kutasababisha Umma uonekane umefanya makosa kuwaamini vijana, jambo ambalo halitarajiwi kutokea.
Pamoja na pomgezi hizo, Katibu wa Shirikisho hilo, amezungumzia masuala mengine ikiwemo changamoto dhidi ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, zinazotokana na utendaji wa TCU na Bodi ya Mikopo. >>>IFUATAYO NI TAARIFA KAMILI


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...