SIMU.tv:  Mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA, yatangaza kuwachukulia hatua kali za kisheria watoa huduma wa mawasiliano watakaoshindwa kulipia madeni wanayodaiwa. https://youtu.be/XWolro6NAZg

SIMU.tv:  Mamlaka ya mapato nchini TRA kwa kushirikiana na jeshi la polisi wafanikiwa kukamata bidhaa mbalimbali za matumizi ya binadamu zilizokuwa zikiingizwa nchini kwa njia zisizo halali kupitia bandari bubu. https://youtu.be/ZkfWp2WZnWk

SIMU.tv:  Halmashauri ya wilaya ya Mtwara vijijini kwa mara ya kwanza yapokea milioni 150 kutoka shirika la maendeleo ya petrol nchini TPDC , ikiwa ni tozo ya uchakataji na usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara hadi Dar es salaam. https://youtu.be/PnqdNHr8GwI

SIMU.tv:  Ujenzi wa daraja la Buguruni uliokwama kwa zaidi ya miezi 8 hatimaye waanza hii leo baada ya mkandarasi mpya kupatikana na kuanza kazi.https://youtu.be/Vew3XEub3hU

SIMU.tv:  Wanafunzi wa shule ya msingi Ipuli iliyoko manispaa ya Tabora wako hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu kufuatia mvua zinazonyesha zilizopelekea kutuama kwa maji. https://youtu.be/RFvt3HiUOgQ

SIMU.tv:  Wananchi wa Zanzibar waadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Rais wa kwanza wa nchi hiyo hayati Abeid Aman Karume na kutaka aenziwe.https://youtu.be/dSyGTlxpRsg

SIMU.tv:  Rais John Magufuli na Mkewe bi Janeth Magufuli waungana na wananchi wa Rwanda kuadhimisha miaka 22 ya mauaji ya kimbari yaliyoua watu milioni 1.https://youtu.be/473D0Sav5ik

SIMU.tv:  Mkuu wa mkoa wa Manyara Joel Bendera amsiamamisha kazi mkurugenzi wa halmashauri ya Hanang kufuatia tuhuma za ubadhilifu.https://youtu.be/YN1_MxnUa2s

SIMU.tv:  Serikali yasema inakusudia kuzifanya hospitali zote za rufaa nchini kuwa chini ya wizara ya afya kutoka TAMISEMI. https://youtu.be/jc4hvDY81QE

SIMU.tv:  Mkutano mkuu wa jumuiya za serikali za mitaa nchini ALAT, wamchagua Gullam Hafeez kuwa mwenyekiti wake mpya kwa kipindi cha miaka 5.https://youtu.be/NNJpsmZmeE4

SIMU.tv:  Shirika la umeme nchini mkoa wa Ilala latoa sababu za kukosekana kwa umeme kwa siku kadhaa huku likidai kuwa ni matokeo ya uchakavu wa miundombinu.https://youtu.be/1Em_yHnk43Y

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...