DSC_0188
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akizungumza jambo kuhusu mradi huo.
Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto, Taasisi ya Graca Machel kwa kushirikiana na serikali imefanya uzinduzi wa mradi ulio na malengo ya kuwarudisha shule watoto 20,000 waishio mkoa wa Mara ambao hawakupata nafasi ya kuwa shuleni.
Akizungumzia mradi huo, Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel alisema taasisi yake imeanzisha mradi huo kwa kutambua kuwa kuna idadi kubwa ya watoto walio nje ya shule kwa sababu mbalimbali hivyo kupitia mradi huo ni matarajio yao kuona watoto wakirudi shule ili kupata elimu ambayo itawasaidia kwa maisha yao ya baadae.
Aliongeza kuwa anatambua kazi aliyoifanya Mwalimu Nyerere kwa kuacha msingi bora wa elimu kwa watu wa aina zote na kuwataka wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanafanikisha mradi kwa kuweka usawa baina ya watoto wa kike na watoto wa kiume ili wote wapate nafasi ya kurudi shule.
“Watoto wanatakiwa wawepo shuleni na wapate elimu bora bila kufanya upendeleo kwa watoto wa kike na watoto wa kiume ili wamalize pamoja elimu ya shule ya msingi na kuendelea na masomo wote wafikie malengo yao,
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo akimshukuru mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel kwa kupeleka mradi huo mkoani kwake.
“Tunataka watoto wasio chini ya 20,000 warudi shule natambua Mwalimu (Nyerere) aliweka msingi bora wa elimu na ni haki ya watoto wote kupata elimu,” alisema Bi. Machel.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo aliishukuru Taasisi ya Graca Machel kwa kupeleka mradi huo mkoa wa Mara na kuahidi kuwa atakuwa kiongozi kufanikisha mradi huo ambao utafanyika kwa kipindi cha miaka miwili.
Pia alitumia fursa hiyo kutoa maagizo kwa watumishi walio chini yake kufanya kazi kwa juhudi katika maeneo yao pindi wanapohitajika kusaidia ili kufanikisha mradi huo ambao una malengo ya kuwasaidia watoto wa mkoa wa Mara kurudi shuleni.
“Nina shukuru sana kwa kuletewa mradi huu na Taasisi ya Graca Machel na nitashiriki kwa asilimia 100 kufanikisha mradi, na nitoe rai kwa watumishi wenzangu kuwa wafanye kazi kwa bidii kuanzia sasa tufanikishe mradi kama umevyopangwa,” alisema Mulongo.
Aidha pamoja na kuzinduliwa kwa mradi huo, pia kunataraji kufanyika utafiti kutazama ni changamoto gani ambazo zilikuwa zinasababisha watoto wa mkoa huo kuwa nje ya shule, utafiti ambao utafanywa na Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF).
DSC_0114
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida akizungumzia utafiti unatarajiwa kufanywa na ESRF kuhusu changamoto ambazo zilikuwa zinasababisha watoto wa mkoa wa Mara kuwa nje ya shule wakati wa uzinduzi wa mradi ulio na malengo ya kuwarudisha shuleni watoto 20,000.
Akizungumzia utafiti huo, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida alisema wanataraji kuanza kufanya utafiti kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itafanyika mwezi huu Aprili na awamu ya pili itafanyika mwezi Julai.
“Utafiti huu ambao unamalengo ya kufanikisha watoto 20,000 wa mkoa wa Mara kurudi shuleni utafanyika kwa awamu mbili, unaanza Aprili kwa maeneo ya Musoma, Bunda, Rorya, Butiama na Wilaya ya Tarime,
“Awamu ya pili itafanyika kuanzia mwezi Julai kwa eneo la Manispaa ya Musoma, Bunda Mjini, Tarime Mjini, Serengeti na Magumu,” alisema Dkt. Kida.
DSC_0290
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akiweka saini ya kuashiria kufanyika kwa mradi huo.
DSC_0296
Watiaji saini ya makubaliano ya mradi huo wakiwa katika picha ya pamoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo.
DSC_0385
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida.
DSC_0378
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi wa mradi huo, Wa kwanza Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida, Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel, Askofu Michael Msongazira wa Kanisa la Roman, Musoma na Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa ESRF, Prof. Fortunata Makene.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...