Afisa Mtendaji Mkuu wa Umoja wa Switch, Danford Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari juu ya utoaji wa huduma za kifedha katika benki leo jijini Dar es Salaam.

UMOJA wa Switch imetimiza miaka 10 katika utoaji wa huduma za kibenki katika kufanya malipo.

Akizungumza leo na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa Umoja wa Switch, Danford Mbilinyi amesema kuwa kati benki 54 wamefikia benki 27 ambazo zinafanya huduma mijini na vijijini.

Amesema kuwa katika utoaji huduma ya umoja switch wameshaweza kuunganisha na kampuni za simu katika utoaji wa huduma kifedha.

Mbilinyi amesema kuwa katika kuongeza huduma ya umoja Switch watu wa  Afrika Mashariki wanaweza kupata huduma za kifedha katika kila nchi.

Aidha amesema kwa mfumo wa malipo ya kidijitali dunia sasa ndio inakwenda huko hivyo itafika wakati kila mtu hatakuwa na fedha za kutembea nazo kutokana  mifumo ya kidijitali kuimarika.

Aidha amesema kuwa umoja switch itazidi kujiimarisha katika utoaji huduma za kifedha katika benki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...