Na Bashir Yakub.
Uhaini ni kosa
la jinai . Ni
kosa kati ya
makosa makubwa ya
jinai. Katika jinai
yapo makosa makubwa
na yapo makosa
madogo. Yumkini udogo
na ukubwa wa kosa waweza
kupimwa kwa kutizama
adhabu ya kosa.
Kosa ambalo huadhibiwa
kwa adhabu ndogo
huwa ni kosa
dogo na lile
ambalo huadhibiwa kwa
adhabu kubwa huwa
ni kosa kubwa.
1.NI SHERIA
IPI HUELEZA MAKOSA
YA JINAI.
Sheria zinazofafanua
makosa ya jinai
zipo nyingi. Hakuna
sheria moja katika
makosa ya jinai.
Hata hivyo sheria
kuu katika makosa
ya jinai ipo. Ni
sheria inayojulikana kama
kanuni za adhabu( penal
code). Hii ni
sheria kuu katika
makosa ya jinai.
Ni sheria inayoeleza
karibia makosa yote ya
jinai. Mbali na
sheria hiyo pia
zipo sheria nyingine kama za
kuzuia na kupambana
na rushwa, sheria ya
uhujumu uchumi, sheria ya
ugaidi na nyinginezo. Hizi
nazo hueleza makosa ya
jinai.
Tofauti kubwa kati ya sheria hizi
na ile ya
kanuni za adhabu
ni kuwa hizi sheria
nyinginezo hueleza makosa
rasmi ya jinai. Kwa
mfano sheria ya
ugaidi itaeleza mambo
ya ugaidi tu
na si vinginevyo, sheria
ya uhujumu uchumi
itaeleza makosa yanayotokana
na uchumi tu na si vinginevyo, sheria
ya utakatishaji fedha
itaeleza utakatishaji fedha
tu na si
vinginevyo.
Wakati sheria
ya kanuni za
adhabu ndani mwake
utakuta makosa tofauti
tofauti ya jinai.
Utakuta makosa ambayo hayafanani na yasiyokuwa na uhusiano.
Utakuta kuhusu kubaka,
kuiba, kupigana, kuua, kuharibu
mali, rushwa, kughushi ,
uhaini na mengine
mengi. Kwahiyo kwa mtu anayehitaji kuyajua
makosa ya jinai
basi na asome sheria
ya kanuni za
adhabu.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...