Wabunge wa bunge la Arika Mashariki, (EALA), kutokaTanzania, wameendelea na ziara yao ya kutembelea vyombovya habari hapa nchini, ikiwa ni mkakati wa Jumuiya hiyo, kushirikisha vyombo vya habari ili kuwafahamishawananchi wa nchi hizo manufaa ya jumuiya hiyo kwao. LeoAprili 13, 2016, wabunge hao wakiongiozwa na Mwenyekiti wao Mh. Makongoro Nyerere, wametembelea kampuni ya The Guardian, wachapishaji wa magazeti ya The Guardian, Nipashe na Lete Raha, na kupata fursa ya kuelezwa shughuli zifanywazo na waandishi wa habarikwenye kampuni hiyo ambapo walitembelea kitengo cha habari mtandao, (E-NEWS), kitengo cha usanifu gazeti na kumalizia kwa mkutano wa kubadilishana mawazobaina ya wabunge hao na uongozi wa chumba cha habari cha The Guardian. Pichani, msanifu wa gazeti la The Guardian, Ben Mgana (aliyekaa), akiwaonyesha jinsi gazeti hilo linavyoandaliwa kabla ya kuchapishwa. Wakwanza kushoto ni Mhari Mtendaji wa gazeti hilo, Wallace Maugo, Mkuu wa chumba cha Habari cha The Guardian, Jesse Kwayu, (wapili kushoto) na wabunge wa hilo wakiongozwa na wmenyekiti wao Mh. Makongoro Nyerere (watatu kulia).NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
MhaririMtendaji wa The Guardian, Wallace Mauggo, (watatu kushoto) na Mhariri Mkuu wa Chumba cha Habari cha The Guardian Limited, Bw. Jesse Kwayu) wakiwaonyesha wabunge hao baadhi ya magazeti yanayochapishwa na kampuni hiyo
Mwenyekiti wa wabunge wa EALA-Tanzania, Mh. Makongoro Nyerere, 9wapili kulia), akisalimianana Mkuu wa kitengo cha habari mtandao (E-NEWS), cha The Guardian Limited, Mashaka Mgeta, wakati wabunge hao walipotembelea chumba cha Habari cha The Guardian Mikocheni jijini Dar es Salaam.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...