Wafanyakazi wa Airtel katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Dodoma, Mbeya na Morogoro leo wameingia katika mitaa mbalimbali katika mikoa yao kuitambulisha huduma mpya ya Airtel Jipimie Yatosha yako kwa wateja na kutoa elimu jinsi ya kufurahia uhuru wa kutengeneza vifurushi vinavyokidhi mahitaji yao
Zoezi hili limefanyika jana katika mkoa wa Dar es salaam ambapo wafanyakazi wa Airtel Makao makuu waliweza kutembelia maeneo mbalimbali na kutoa elimu hiyo, halikadhalika timu ya Airtel imefikia wateja wake kupitia vyombo vya habari mbalimbali ikiwemo radio, Tv na mitandao ya kijamii kwa lengo la kuwahabarisha wateja na watanzania kwa ujumla juu ya huduma hiii ya kipekee, kibunifu na ya kwanza nchini Tanzania inayomuwezesha wateja kununua kifurushi cha muda wa maongezi tu, au kuchanganya kifurushi cha muda wa maongezi na MB za intaneti au Muda wa Maongezi na SMS lakini pia bado wanaweza kupata vifurushi vyote yaani muda wa maongezi zaidi, SMS zaidi na MB zaidi. Vifurushi hivi vinapatikana kwa siku, wiki au mwezi
Ili kujiunga na kufurushi cha Airtel jipimie yatosha yako mteja anatakiwa kupiga *149*99# kisha kufata maelekezo.
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mwanza wakitoa elimu kwa wakazi Mwanza mjini na wafanyabiasharaa waendesha Bodaboda kuhusu huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake.
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuingia mtaani kukutana na wateja na kuitambulisha huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kujitengenezea vifurushi vya yatosha wanavyovitaka
Wafanyakazi wa Airtel Mkoani Morogoro wakishuka kutoka kwenye basi kwenda kukutana na wateja katika maeneo yao ya kazi ili kutambulisha huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kutengeneza vifurushi vya yatosha wanavyovitaka
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akifanya mahojiano na Jembe radio mkoani Mwanza na kutoa elimu kwa wasikilizaji wa vipindi vyake juu ya huduma mpya ya kibunifu ya Airtel jipimie yatosha yako itakayowawezesha wateja kutengeneza vifurushi vya yatosha wanavyovitaka
Wafanyakazi wa Airtel mkoani Arusha wakiongea na wateja sokoni na kutoa elimu jkuhusu huduma mpya ya kifurushi cha Airtel Yatosha kijulikanacho kama “Jipimie Yatosha Yako” kitakachompatia uhuru mteja kutengeneza na kununua kifurushi kinachokidhi mahitaji yake.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...