Teresia Mhagama na Asteria Muhozya

Imeelezwa kuwa, Wizara ya Nishati na Madini imeendelea kurahisisha utoaji wa huduma za leseni za madini ambapo sasa  wamiliki wa Leseni hizo wanaweza  kupata taarifa za ada ya leseni kwa njia ya ujumbe wa simu (SMS).

 Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA katika Wizara ya Nishati na Madini, Francis Fungameza alisema kuwa ili mteja aweze kupata huduma hiyo anatakiwa kuandika neno MEM, ache nafasi , kisha aandike  Namba ya Leseni na kutuma kwenda 15341.

Fungameza alisema kuwa hizo ni habari njema kwa wamiliki wa leseni kwani sasa wataweza kupata  taarifa hizo kwa wakati na hivyo  kulipia ada za  leseni hizo kwa wakati.

Aidha Fungameza alisema kuwa Wizara imekuwa ikibuni njia mbalimbali ili kuhakikisha kuwa huduma za utoaji wa leseni za madini pamoja na taarifa mbalimbali kuhusu leseni hizo zinapatikana kwa urahisi na uharaka tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...