Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewaongoza zaidi ya wasanii na wadau wa Sanaa mia moja katika maadhimisho ya siku ya Jazz duniani yaliyofanyika makao makuu ya Baraza hilo yaliyoko Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam.

Maazimisho hayo ambayo yameazimishwa kwa mara ya kwanza nchini yalipambwa na burudani mbalimbali kutoka kwa Bendi ya muziki wa Jazz huku wataalam na wasanii wakongwe wakiwasilisha mada mbalimbali katika kongamano maalum lililobeba mijadala na hoja mbalimbali kuhusu muziki huo.

Akizungumza kwenye kongamano hilo Msanii Mkongwe John Kitime alisema kuwa muziki wa jazz una historia ya aina yake duniani hasa katika kujenga diplomasia baina ya mataifa, kuunganisha tamaduni mbalimbali duniani na kushiriki katika ukombozi dhidi ya ukandamizaji na utumwa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza akizungumza na wadau wa Sanaa kwenye maadhimisho ya Siku ya Muziki wa Jazz duniani yaliyofanyika mapema wiki hii katika Ukumbi wa Baraza hilo ulioko Ilala Sharif Shamba jijinI Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Msanii mkongwe John Kitime na Mkuu wa Kitengo cha Matukio kutoka BASATA Kurwijira Mareges.

“Sifa kubwa ya muziki huu wa jazz ni namna ulivyopokelewa na kuvuka mipaka katika tamaduni mbalimbali. Ni muziki unaoeleza hisia na matukio ya kweli yanayotokea. Ni aina ya muziki ambao ni urithi wa Dunia kwani una mchango wa pekee” alisema Kitime.

Awali akielezea historia ya muziki huu, Mtaalam wa muziki ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Matukio kutoka BASATA Kurwijira Mareges alieleza kwamba muziki wa jazz una mizizi yake barani Afrika kabla baadaye kupitia biashara ya utumwa haujasambaa sehemu mbalimbali duniani na kugeuka urithi wa Dunia nzima.
Msanii mkongwe na mchambuzi wa masuala ya Sanaa John Kitime akifafanua juu ya kwa nini bendi nyingi nchini zilitumia jina la jazz wakati akiwasilisha mada kwenye maadhimisho ya siku ya muziki wa Jazz duniani yaliyofanyika Ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ulioko Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam. Wengine kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza, Mwakilishi kutoka UNESCO Maximilan Chami na Afisa Habari wa BASATA Aristides Kwizela

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...