Na  Bashir  Yakub
Sheria  ya  Ajira  na  Mahusiano  Kazini  ya 2004 ndiyo  sheria  mama  katika  masuala  ya  ajira. Kwa  anayetaka  kujua  haki  na  wajibu  wa kazi  na  mfanyakazi,  mwajiri  na  mwajiriwa  basi  na  asome  sheria  hii.  Sheria  hii  ilianza kutumika  rasmi tarehe  5/ 1/  2007.

Misingi  mikuu  ya sheria  hii  ni  usawa  wa  ajira kwa  jinsia, ujira  unaolingana  na kazi  inayofanywa  na  mfanyakazi, haki  na  maslahi  bora  kwa  mfanyakazi, mazingira  bora  na  salama  ya  kazi  na  mengine  mengi  hasa  yanayoshabihiana  na  haki  za  binadamu.

Kumwachisha  kazi  mfanyakazi  ni  moja  ya  maeneo  muhimu  katika  sheria  hii. Wakati  gani  mfanyakazi  aachishwe  kazi,  kwa  kosa  gani, utaratibu wa  kumwachisha  kazi,  stahiki  zake  baada  ya  kuachishwa  kazi,  uachishwaji  kazi  haramu, utaratibu  wa  hatua  za  kuchukua  panapo  uharamu  katika  kuachishwa  kazi  ni  sehemu ya  mambo  muhimu  katika  sheria  hii.
Makala  haya  yataeleza  habari  hii  ya kuachishwa  kazi  lakini  yatalenga  kipengele  kimoja  tu  cha  uhalali wa  kumwachisha  mfanyakazi  kwa kosa  la  kwanza.
1.NI  IPI  TAFSIRI  YA  KUACHISHWA  KAZI.
Kuachishwa  kazi  ni  hatua  ambapo  muajiri  husitisha  mkataba  wa  ajira  kwa  notisi  au  bila  notisi  kwasababu  mbalimbali  zikiwemo  za  utovu  wa nidhamu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...