Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Belize Bw. Wilfered Eliringron wakati Makamu wa Rais alipowasili katika Hoteli ya Airways mjini Papua New Guinea. Makamu wa Rais yupo Nchini Papur New Guinea kwa ajili ya kumwakilisha Rais John Magufuli katika mkutano wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho utakaojadili masuala ya kukuza Usawa na Maendeleo endelevu kwa ajili ya Wananchi wa Nchi wanachama kuimarisha majukumu ya Nchi za ACP katika Utawala Bora na Maendeleo, Usalama na Utulivu wa kisiasa. Mkutano huo utahudhuriwa na Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mwandaaji Mkuu wa mkutano wa The HL MEETING UN WOMEN unaotarajiwa kufanyika keshokutwa mjini Guinea, Makamu wa Rais Makamu wa Rais yupo Nchini Papur New Guinea kwa ajili ya kumwakilisha Rais John Magufuli katika mkutano wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho utakaojadili masuala ya kukuza Usawa na Maendeleo endelevu kwa ajili ya Wananchi wa Nchi wanachama kuimarisha majukumu ya Nchi za ACP katika Utawala Bora na Maendeleo, Usalama na Utulivu wa kisiasa. Mkutano huo utahudhuriwa na Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP). (Picha na OMR Papua New Guinea).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 31, 2016

    Hii mikutano ya kuhadili namna ya utekelezaji wa malengo ni danganya toto tu. Leo hii hakuna asiyejua cha kufanya kutekeleza. Kinachohitajika ni fedha tu. Waliotunyonya siku nyingi leo hawana fedha. Hiyo inayodaiwa kuwa eti ni misaada hata kwao huko matatizo kibao. Hivi tunahitaji safari kama hii ya kujadili eti "masuala ya kukuza Usawa na Maendeleo endelevu kwa ajili ya Wananchi wa Nchi wanachama kuimarisha majukumu ya Nchi za ACP katika Utawala Bora na Maendeleo, Usalama na Utulivu wa kisiasa" Huhitaji kuwa Profesa kujua majibu ya hilo. Ndio maana Rais Magufuli amefanya vyema kutohudhuria makongamano haya ya maneno tupu. Fedha ya safari hii ingejenga shule ya msingi ama kulipia waalimu wa wanafunzi kule UDom. Hebu tubadilike tumsaidie Magufuli na tuisaidie nchi yetu. Sio kila kitu Magufuli pekee ndio apige kelele.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...