Pichani Mdau Othman Mangube akiwa sambamba na mkewe Bi Mariam Swedy wakiwa katika nyuso za furaha,mara baada ya kufunga ndoa yao hapo mwaka jana,ambapo leo Wanamshukuru Mungu kwa kuvuka milima na mabonde mengi katika mazingira tofauti tofauti ya maisha na sasa Wanatimiza mwaka mmoja wa Ndoa yao,ambayo wao bado wanaamini ni changa,lakini kwa rehma na baraka za Mwenyezi Mungu atawasimamia na kuwaongoza katika mstari ulio nyoofu na kuwafikisha miaka mingi zaidi.

"Pia tunawakia heri ndugu jamaa na marafiki popote pale mlipo,tunawashukuru sana kwa ushirikiano wenu mlioutoa wakati wa kuifanikisha ndoa hii,nawashukuru sana na tuendelee na ushirikiano huo,sina cha kuwalipa lakini Mwenyezi Mungu atawalipa zaidi."Asanteni sana
Bwana Othman Mangube akiwa na Mkewe Bi Mariam Swedy katika pozi la picha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...