Shule ya Msingi Ulonge iliyopo katika Manispaa ya Iringa takriban  kilometa 10 kutoka Iringa Mjini, imepokea jumla ya madawati 30 kutoka kwa mdau wa maendeleo Bw.Suhail Ismail Thakore (pichani kulia) wa Manispaa ya Iringa.

Awali shule ilikuwa na uhitaji Wa madawati 37, hivyo baada ya kupokea madawati hayo, mahitaji yatakuwa 7. Na baada ya kuwepo madawati 6 mabovu ambapo yakikarabatiwa hayo 6 uhitaji Utakuwa ni dawati moja. 
Thamani ya madawati hayo 30 ni shilingi 1,800,000/-.Shule ya Ulonge ina jumla ya wanafunzi 495 walimu 9.


 Sehemu ya madawati yaliyotolewa na mdau wa maendeleo Bw.Suhail Ismail Thakore 
Mdau wa maendeleo Bw.Suhail Ismail Thakore  wa Manispaa ya Iringa akiwa na walimu wa shule hiyo baada ya kutoa msaada wa madawati hayo 30.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...