Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Amani K. Mwenegoha ameagiza maafisa tarafa kusimamia kwa karibu shughuli za hifadhi ya mavuno yaliyopatikana katika Mvua za vuli Msimu wa 2015/2016 kwa kuhamasisha wananchi wenye mavuno mengi kila mahali kuhifadhi vizuri ili mavuno hayo yasiharibike na kuweka akiba ya kutosha kwaajili ya kaya zao.

Pia ameagiza Wakulima washauriwe kuuza ziada tu ya mavuno yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao muhimu na kila kaya isimamiwe kuhakikisha imehifadhi mazao ya chakula cha kuwatosha huku akiagiza Wafugaji washauriwe kuvuna sehemu ya mifugo yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao muhimu na kununua nafaka kwaajili ya kaya zao.

Amesisitiza maelezo haya yawafikie viongozi ngazi za kata,vijiji na vitongoji kwaajili ya utekelezaji na taarifa iwasilishwe kwa Mkuu wa Wilaya kabla ya 13/05/2016.

Imetolewa na

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bukombe
Geita 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...