Na Tiganya Vincent_MAELEZO-Dodoma.

Serikali kwa kushirikiana na wadau wa ndani na nje ya Nchi wameifanyia maboresho Sera ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya mwaka 2003 na kuja ya sera mpya ya mwaka 2016 ili kuunganisha sekta muhimu za uzalishaji na viwanda katika miundombinu ya TEHAMA.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Injinia Edwin Ngonyani wakati wa uzinduzi wa Sera ya Tekonolojia ya Habari na Mawasiliano ya mwaka 2016.


Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuiwezesha Tanzania kutumia fursa zinatokana na uwepo wa miundombinu ya TEHAMA kuingia katika uchumi wa kati ifakapo 2025 kwa kuimarisha matumizi ya TEHAMa katika sekta mbalimbali za uzalishaji nchini.


Mhe. Ngonyani aliongeza kuwa Sera hiyo ni muhimu katika kujenga jamii habari itakayowezesha nchi kufikia maarifa yatakayosaidia kwenda sanajari na mpango wa Taifa kujenga uchumi wa viwanda.

Alisema kuwa Sera hiyo imejikita katika kukuza matumzi TEHAMA katika uzalishaji ili kuongeza tija , kukuza utafiti na kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi katika TEHAMA kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Awali akiongea kabla ya uzinduzi wa Sera hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(Mawasiliano) Profesa Faustin Kamuzora alisema kuwa Sera hiyo itasaidia kuongeza ufanisi wa utendaji wa kazi wa kila siku katika sekta mbalimbali nchini.


Alisema kuwa sera hii itasiaidia kwenda sanajari ya ukuaji wa kasi wa matumzi ya mawasiliano hapa nchini.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Injinia Edwin Ngonyani (wa pili kulia) akizindua Sera ya Taifa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya mwaka 2016 leo mjini Dodoma. Wengine ni Mwakilishi wa Balozi wa Finland nchini Oscar Kassy(kulia) , Katibu Mkuu wa Wizara hiyo aliyeshughulikia mawasiliano Profesa Faustin Kamuzora( wa pili kushoto) na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Rehema Madenge(kushoto). 
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Injinia Edwin Ngonyani akiwahutubia wadau wa TEHAMA wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya mwaka 2016 leo mjini Dodoma.
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na wadau wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Injinia Edwin Ngonyani wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya mwaka 2016 leo mjini Dodoma.
Kupata hotuba ya Waziri BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...