MAREHEMU JACKLINE OSWALD KAPINGA
Familia ya Marehemu Mzee Oswald Kapinga ya Sinza - Dar e salaam (karibu na White inn) inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Jacqueline kilichotokea jana tarehe 29/05/2016 katika hospitali ya muhimbili jijini Dar es salaam.
Familia inapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ya kuwa, msiba utakuwa nyumbani kwa wazazi wake hapo hapo kwao sinza.
Taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika. Taarifa ya awali kutoka kwa familia, Marehemu wanategemea kumuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele kesho Jumanne Tarehe 31/05/2016 katika makaburi ya sinza karibu na Ukumbi wa mwika kuanzia saa 8.00 Mchana.
Kwa taarifa zaidi na maelekezo mbali mbali unaweza kuwasiliana na makaka wa marehemu hapo chini:
JOSEPH O. KAPINGA (Mwananchi communication) -0788617654
GOSBERT O. KAPINGA - 0754286301
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA,
JINA LAKE LIHIMIDIWE
- AMEN.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...