Na Chalila Kibuda,
Globu ya Jamii.
MAMLAKA ya Mapato
Nchini (TRA) kwa mwezi uliopita imekusanya Sh.Trioni
1.035 ambayo ni sawa na asilimia 99
.5 ya lengo kukusanya sh.trioni 1.040 .
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es
Salaam, Kamishina Mkuu wa TRA, Bw. Alphayo Kidata amesema kuwa katika makusanyo ya
miezi 10 wameweza kukusanya sh. Trioni 10.92 ambayo sawa na asilimia 99 ya lengo ya
sh.trioni 11.02 katika lengo la kipindi
hicho.
Amesema kuwa TRA imedhamiria kukusanya zaidi ya sh. Trioni 1.4 na kuvuka
lengo la mwaka wa fedha wa 2015/2016 katika
miezi miwili ya kumaliza mwaka wa fedha
ambalo ni sh. Trioni 12.3.
Bw. Kidata amesema kuwa TRA itaendelea na jitihada mbalimbali kuhakikisha inafikia lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2015 / 2016 licha kuwepo kwa changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo.
Bw. Kidata amesema kuwa TRA itaendelea na jitihada mbalimbali kuhakikisha inafikia lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2015 / 2016 licha kuwepo kwa changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo.
Amesema kuwa wananchi
wamejua umuhimu wa kodi na kuanza kutoa ushirikiano katika kudhibiti
mianya ya magaendo, pamoja na kuziba mianya ya upotevu wa mapato ikiwa katika
usimamizi wa mifumo ya mlipa kodi kulipa kodi anayostahili bila usumbufu
wowote.
Kamishina Mkuu amesema
kuwa wamewakamata wafanyabiashara 300 kwa kuwatoza faini zaidi ya sh. Milioni 746
kwa makosa ya kutotoa risti, kutoa risti zenye bei pungufu pamoja na kutotumia
mashine za Kieletroniki na baadhi yao
walihukumiwa kifungo au kulipa faini .
"TRA haitawavumilia wafanyabiashara wanayoikosesha serikali mapato kwa kuuza na kutoa huduma bila risti kwa makusudi yao kamwe hawataachwa", alisisitiza Bw. Kidata.
"TRA haitawavumilia wafanyabiashara wanayoikosesha serikali mapato kwa kuuza na kutoa huduma bila risti kwa makusudi yao kamwe hawataachwa", alisisitiza Bw. Kidata.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...