Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, (wa nne kutoka kushoto) akiungana na wafanyakazi wanaounda Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kuimba wimbo wa mshikamano daima, wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza hilo uliofanyika Mjini Morogoro Mwishoni mwa juma. kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Dorothy Mwanyika na kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu Amina Hamis Shaban.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akihutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo (hawako pichani) mjini Morogoro, ambapo amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kufanyakazi kwa bidii na kuacha mazoea ili kutimiza malengo ya kukusanya mapato na kusimamia matumizi yake kikamilifu.
Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Cyprian Kuyava, akitoa neno la shukrani mjini Morogoro, baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka mitatu ijayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...