Kufuatia Uongozi wa Klabu ya Yanga kuwatangazia washabiki wao kwamba Mechi ya Timu yao dhidi ya TP Mazembe ya Nchini Congo inayopigwa leo katika dimba la Taifa, kuwa haitakuwa na viingilio, Mapema asubuhi hii Mashabiki hao wamejitokeza kwa wingi na kupanga foleni katika mageti yote ya kuingilia uwanjani hapo kusubiria kuanza kwa utaratibu wa kuingia uwanjani hapo kwa lengo moja la kuipa nguvu timu yao, inayoshiriki katika Mashindano ya Kombe la Shirikisho. Ripota wa Globu ya Jamii ambaye yupo Uwanja wa Taif hivi sasa, anaeleza kuwa Mashabiki hao walianza kujitokeza kuanzia saa 12 asubuhi, huku wengine wakisema kuwa wameamua kuja mapema ili kuujaza uwanja na kutowapa nafasi watani wao ambao inadaiwa kuwa walisema wataiunga mkono hiyo timu ya kigeni.
 Hapa mageti yakifunguliwa tu, watu ndani.
 Msururu wa Washabiki wa Yanga nje ya Uwanja wa Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 28, 2016

    hivi hawa watu hawana kazi au ndo mapenzi ya timu yetu tu haya .saa moja asubuhi wako kiwanjani mechi ni saa tisa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...