Mkurungezi Mtendaji wa benki ya PBZ, Juma Ameir Hafidh,akizungumza na wafanyakazi na Familia zao wakati futari iliyoandaliwa na benki ya PBZ katika Hoteli Hyaat Regency jijini Dar es Salaam.
Mwanafamilia wa Benki hiyo, Abdul Juma akisoma dua baada ya kufuru katika futali futari iliyoandaliwa na benki katika Hoteli Hyaat Regency jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wafanyakazi na familia zao `pamoja na wageni waalikwa wakiwa katika wakati wa kuchukua futari iliyoandaliwa na benki ya PBZ katika Hoteli Hyaat Regency jijini Dar es Salaam.
BENKI ya PBZ inatarajia kuanza kutoa mikopo kwa wajasiriamali ifikapo Septemba mwaka huu.
Akizungumza wakati wa hafla ya futari iliyowakutanisha wafanyakazi wa PBZ na familia zao, Mkurungezi Mtendaji wa benki hiyo, Juma Ameir Hafidh, alisema kwamba kazi ni ibada hivyo kila mmoja.
Aliwataka wafanyakazi hao kuheshimu fedha pamoja na kutolewa madaraka ikiwemo kumuogopa Mungu ili wasiwe na tamaa na wakaiba.
Akizungumzia PBZ Mkurugenzi huyo alisema kwamba, kuanzia Julai mosi mwaka huu wataanza mchakato wa kuhakikisha Septemba wanatoa mikopo ya vitu kwa wajasiriamali ili kuwasaidia kukua kiuchumi.
PBZ pia imewataka wafanyakazi wake kuongeza juhudi, nidhamu, upendo na ari katika kazi kwani ndiyo siri ya mafanikio.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...