Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu ya Simba na Toto African ya Jijini Mwanza, Edward Christopher amesaini mkataba wa mwaka mmoja na timu ya Kagera Sugar baada ya kumalizana na  Toto mwishoni mwa msimu huu huku timu hiyo ikifanikiwa kusalia ndani ya ligi msimu ujao na  aliweza kuisaidia timu hiyo kukusanya alama 30 katika msimamo wa ligi huku wakifunga magoli 26 na Kabla ya kumalizika kwa ligi msimu huu mchezaji huyo alikuwa mguu ndani mguu nje kuachana na timu hiyo.

Edward amesema kuwa ameamua kuingia mkataba na timu hiyo baada yaw kukubaliana katika baadhi ya matakwa yake huku akiahidi kuitumikia kwa juhudiw zake zote na toka awali alishasema atafanya kazi na timu yoyote itakayokuwae tayari kukubaliana na matakwa yake lakini nafasi kubwa akiipa Toto.

"Nilikuwa tayari kufanya kazi na timu yoyote msimu ujao ili mradi tu tukubaliane na wawe tayari kunipa kile ninachokitaka", amesema Eddo.

Kwa sasa ataendelea na mazoezi ili kuhakikisha Kagera hawajuti kumjumuisha ndani ya kikosi chao na anachokisubiri ni ripoti ya kambi ya timu hiyo ili kuanza kambi rasmi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu.

Mshambuliaji huyo ni moja ya zao la Simba lakini alishindwa kuendelea baada ya uongozi kutokuwapa nafasi katika kikosi hata baada ya kuonesha uwezo mzuri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...