Naibu Waziri, Ofisi  ya  Waziri Mkuu, Mhe. Dr. Abdallah Possi ( Mb) akizungumza wakati wa majadiliano ya jumla kuhusu  utekelezaji wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu. Mhe. Possi anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tisa  wa Nchi  Wanachama  wa Mkataba  wa Watu  Wenye Ulemavu. Mkutano huu wa siku tatu umeanza siku ya  Jumanne hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.  Wajumbe wengine katika  picha ni kutoka kushoto Mhe. Stella Ikupa Alex ( Mb), Mhe. Riziki Said Lulida ( Mb) na Mhe Elly Marko Macha ( MB). 
Ujumbe wa Tanzania wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa  Tisa wa Mkataba wa Watu  Wenye  Ulemavu,  ufunguzi wa mkutano  huu  ulifanyika katika  Ukumbi Mkuu wa Mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Mkutano huu wa siku tatu ajenda yake ni "Utekelezaji wa  Agenda  ya Maendeleo Endelevu ( Agenda 2030) Kwa Watu Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”. Unahudhuriwa na  Washiriki kutoka nchi 164   ambazo zimeridhia  Mkataba huu, Asasi zisizo za kiserikali pia  zinahudhuria katika  mkutano  huu ambao ni  maalum kwa watu wenye ulemavu wa aina zote. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...