Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Felix Lyniva wakifuatilia mada katika mafunzoa ambapo Halmashauri za Wilaya zao za Butiama na Rorya mkoani Mara ndio zimechaguliwa kuwa za kwanza kuanza utekelezaji wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za umma(PS3) katika sekta za afya, elimu na kilimo.
HALAMSAHAURI Za Wilaya ya Rorya na Butiama mkoani Mara zimechaguliwa kuwa za kuanza utekelezaji wa mradi Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) chini ya ufadhili wa Shirika la Maemdeleo la Kimataifa la Marekani (USAID).
Tayari watendaji kutoka halamshauri husika wanapatiwa mafunzo ya siku moja leo na wiki ijayo madiwani wao nao watapatiwa mafunzo maalum ya namna ya kushiriki utekelezaji wa mradi huo. Mafunzo hayo ya wiki moja yatafanyika mjini Bunda. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...