RPC Ilala Salum R. Hamduni
Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama tumejipanga ipasavyo kuhakikisha mchezo huo wenye mvuto mkubwa kwa washabiki wa Tanzania, nchi za Afrika mashariki na Afrika nzima kuchezwa katika hali ya usalama.
Aidha tunaomba wananchi wasiwe na shaka yoyote ya kiusalama na pia watupe ushirikiano wa kutoa taarifa kwa jambo lolote watakaloliona kuwa linaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa nje au ndani ya uwanja. 
Kutakuwa na CCTV Camera ili kuhakikisha sehemu zote mageti ya kuingilia na kutokea na maeneo yote yanaonekana na kuweka kumbukumbu za matukio yote.
Pamoja na hayo wananchi wanatakiwa kuwa watulivu katika kushangilia mechi hiyo, na kuepuka kufanya mambo yafuatayo:

·        Kuingia na chupa za kimiminika cha aina yeyote,
·        Kuingia na silaha ya aina yoyote
·        Kupaki magari ndani ya uwanja
·        Kukaa sehemu ambazo tiketi zao haziwaruhusu.
  
SALUM. R. HAMDUNI
KAMANDA WA  POLISI MKOA IALA

DAR ES SALAAM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...