Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Sihaba Nkinga, akisalimiana na mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Diwani Thadey S. Massawe (kushoto), baada ya kupokea Maandamano ya wadau walioshiriki Maadhimisho ya Siku ya Wajane Duniani mwaka 2016 mkoa wa Dar es salaam, yaliyoandaliwa na asasi ya TAWIA na kufanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es salaam, tarehe 23 Juni, 2016.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Sihaba Nkinga akihutubia wadau wa utetezi wa haki za wajane mkoa wa Dar es salaam (hawapo pichani) waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Wajane Duniani mwaka 2016 yaliyoandaliwa na Shirika Lisilokuwa la Kiserikali la TAWIA yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es salaam, tarehe 23 Juni, 2016.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Sihaba Nkinga (wa pili kulia) , akifuatilia ushuhuda wa mama mjane (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wajane Duniani mwaka 2106 katika mkoani wa Dar es salaam, wa kwanza kushoto ni mwakilishi wa UN Bibi Chitrahekha Massey, wa pili kushoto ni mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Diwani Thadey S. Massawe, na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa asasi ya TAWIA Bibi Rose Sarawatti, yaliyoandaliwa na asasi ya TAWIA katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es salaam, tarehe 23 Juni, 2016.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Sihaba Nkinga, akionesha kuridhishwa na ubora wa bidhaa zinazouzwa zinazouzwa na wanawake wajane, wakati alipotembelea mabanda ya Maonesho wakati wa kilele cha Madhimisho ya Siku ya Wajane Duniani mkoa wa Dar es salaam, yaliyoandaliwa na asasi ya TAWIA katika viwanja vya Mnazi mmoja, jijini Dar es salaam, tarehe 23 Juni, 2016.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...