Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii
KOCHA mkuu wa Yanga, Hans Van De Pluijm amesema kuwa ana imani na kikosi chake kuwa kitacheza vizuri kwani ameweza kukaa nao kwa siku kadhaa na amewapa mbinu mbalimbali hasa wanapokuwa wapo ugenini na zaidi amewataka kutokufuata mchezo wa wapinzani wao.
Pluijm amesema hayo kupitia kwenye mtandao wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na kusema wameenda nchini Algeria kwa ushindi ila hawatataka kupoteza mchezo huo zaidi ushindi ndio wanachokitaka au kupata sare ambayo itakuwa na manufaa kuliko kupoteza kabisa.
"Siku chache nilizokaa na wachezaji na wakafanya mazoezi ya pamoja yanatosha kabisa kuweza kuondoka na ushindi kwani Nimewaambia wacheze mchezo wetu na zaidi wasiwafuate mchezo wao,"amesema Pluijm. Ninachoamini kuwa wachezaji wangu watafuata kile nachowaambia na zaidi wapinzani wangu watatumia uwanja wao wa nyumbani kucheza kwa kujiamini na sisi tutacheza kwa tahadhari kubwa sana.
Yanga wanacheza leo na Mo Bejaia ikiwa ni mchezo wa ufunguzi wa kundi A ambao utapigwa nchini Algeria saa sita na robo usiku wa saa za Afrika Mashariki. Katika mchezo huo watakosa huduma ya Nahodha wao Nadir Haroub 'Canavaro' anayetumikia kadi nyekundu na Juma Abdul ambaye ni majeruhi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...