Frank Mvungi-Maelezo.
MAAFISA Maendeleo ya jamii walioajiriwa katika Halmashauri hapa nchini wameongezeka kutoka 1,855 mwaka 2005 hadi kufikia 2,675 ikiwa ni ongezeko la asilimia 44 hali inayosaidia kuboreshwa kwa huduma za jamii.
Kauli hiyo imetolewa Leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia vyuo vya Maendeleo ya Jamii Bi. Neema Ndoboka toka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake Wazee na Watoto wakati wa Mkutano na Vyombo vya Habari uliolenga kueleza mafanikio yaliyofikiwa na Wizara hiyo katika kukuza Sekta ya Maendeleo ya Jamii hapa nchini.
Akifafanua Bi. Neema amesema kuwa chuo cha Maendeleo ya jamii Tengeru kimepandishwa hadhi kuwa Taasisi ya Elimu ya Juu inayotegemea kiutendaji hali itakayosaidia kuongeza kiwango wa Maafisa Maendeleo ya Jamii wanaohitimu katika chuo hicho.
Pia Bi. Neema amesema kuwa vyuo vinavyosimamiwa na Wizara hiyo vinatoa wahitimu wanaokidhi mahitaji ya soko la ajira kutokana na umahiri na uzoefu wanaojengewa wakiwa vyuoni.
Aidha wahitimu wa Kidato cha nne na kidato cha sita wenye utashi katika fani ya maendeleo ya jamii wanakaribishwa kutuma maombi yao kwenye “Central Admission System” (CAS),kupitia www.nacte.go.tz.
Taaluma ya Maendeleo ya Jamii inatolewa kwa kuzingatia taratibu na Kanuni zinazotolewa na kusimamiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).hivyo NACTE inasimamia uandaaji wa mitaala inayotumika katika utoaji wa mafunzo,muda wa masomo,mitihani na Vigezo vyake,pamoja na ubora wav yeti wanavyotunukiwa wahitimu kwa kila ngazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...