Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (aliyeketi kulia) na Makamu wa Rais wa Chuo cha Utawala China Bw. Chen Li (aliyeketi kushoto) wakisaini hati za makubaliano ya ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili mapema leo jijini Dar es Salaam. Katika makubaliano hayo, Chuo cha Utawala China kitatoa fursa kwa watumishi wa umma nchini Tanzania kwenda kupokea mafunzo ya kiutawala nchini China, pamoja maandalizi ya makongamano tofauti tofauti na utoaji wa mihadhara kuhusu utawala, maendeleo ya majiji na ‘Kufahamu zaidi China’ yatakayofanyika hapa nchini na China.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (kulia) na Makamu wa Rais wa Chuo cha Utawala China Bw. Chen Li (kushoto) wakibadilishana hati za makubaliano ya ushirikiano baada ya kusaini hati hizo mapema leo jijini Dar es Salaam zenye malengo ya kutoa mafunzo ya kiutawala kwa watumishi wa umma nchini.
Ujumbe kutoka Chuo cha Utawala China na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Uongozi wakiendelea na mazungumzo wakati wa tafrija fupi ya utiaji saini ya hati za makubaliano kati ya Taasisi hizo mbili zenye malengo ya kuongeza ufanisi serikalini kupitia mafunzo kwa watumishi wa umma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...