Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Global Publishers imezindua huduma itakayowawezesha wateja wake kupata habari kuhusu wasanii mbalimbali kila siku kwa njia ya SMS. 
Kwa shillingi 100 tu kwa siku, mteja atakayejiunga na huduma hii ataweza kupata habari mbalimbali kuhusu msanii atakaemchagua. 
Ili kujiunga na huduma hii, mteja anatakiwa kutuma neno ambalo ni jina la msanii wake pendwa, mfano Lady Jaydee au Ali Kiba kwenda namba 15542. 
“Huduma hii inaleng kuwaunganisha wateja wetu na wasanii wao pendwa, tunataka kuwaweka karibu. Na hii ni moja ya jitihada zetu kabambe za kutumia teknolojia kurahisisha na kufanya maisha kuwa murua kwa wateja wetu na hivyo kuwapa uwezo wa kupata habari zinazohusu wasanii wao kupitia simu zao za mkononi,” alisema Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu.

Aliongeza kuwa ingawa huduma hii imeunganishwa moja kwa moja, mteja bado anao uwezo wa kujiondoa wakati wowote. 
Mkurugenzi wa Global Publishers, Abdallah Mrisho alisema wanatarajia kutumia nafasi hii kutoka Vodacom Tanzania kuwapa wasomaji wao habari zinazowahusu wasanii wao pendwa kwa njia ya simu. 
Mpaka sasa huduma hii ina wasanii nane ambao ni Alikiba, Lady Jaydee, Kajala, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel, Jacqueline Wolper, Shilole and Rose Ndauka. 
Vodacom Tanzania na Global Publishers imeahidi kuongeza wasanii wengi zaidi kwenye huduma hii. 


























 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akifurahia jambo na Msanii wa bongo movies Auntie Ezekiel na wasanii wengine Kajala Masanja, Shilole”Shishi Baby” na Mkurugenzi wa Global Publishers, Abdallah Mrisho wakati wa Uzinduzi wa huduma  ya kutoa habari za ‘Papo Hapo’ za wasanii mbalimbali  kila siku kwa njia ya SMS kwa kushirikiana na Global Publishers. Ili kujiunga na huduma hii mteja  wa mtandao huo anatakiwa kutuma neno ambalo ni jina la msanii wake pendwa, mfano Lady Jaydee au Ali Kiba kwenda namba 15542 na kukatwa shillingi 100 tu  kwa siku. 
 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(wapili kulia)akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa Uzinduzi wa huduma  ya kutoa habari za ‘Papo Hapo’ za wasanii mbalimbali  kila siku kwa njia ya SMS kwa kushirikiana na Global Publishers. Ili kujiunga na huduma hii mteja  wa mtandao huo  anatakiwa kutuma neno ambalo ni jina la msanii wake pendwa,  kwenda namba 15542. Na kukatwa shillingi 100 tu  kwa siku.Kutoka kushoto Msanii wa Bongo Movies Auntie Ezekiel,Kajala Masanja na Mkurugenzi wa Global Publishers, Abdallah Mrisho.

 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(wapili kushoto)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa Uzinduzi wa huduma  ya kutoa habari za ‘Papo Hapo’ za wasanii mbalimbali  kila siku kwa njia ya SMS kwa kushirikiana na Global Publishers. Ili kujiunga na huduma hii mteja  wa mtandao huo anatakiwa kutuma neno ambalo ni jina la msanii wake pendwa, mfano Lady Jaydee au Ali Kiba kwenda namba 15542. Na kukatwa shillingi 100 tu  kwa siku,Kutoka kushoto ni Msanii wa Bongo movie,Kajala Masanja, Mkurugenzi wa Global Publishers, Abdallah Mrisho na Shilole”Shishi Baby”.
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Shilole”Shishi baby”akiofafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa huduma  ya kutoa habari za ‘Papo Hapo’ za wasanii mbalimbali  kila siku kwa njia ya SMS kupitia mtandao wa Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Global Publishers. Ili kujiunga na huduma hii mteja  wa mtandao huo  anatakiwa kutuma neno ambalo ni jina la msanii wake pendwa,  kwenda namba 15542. Na kukatwa shillingi 100 tu  kwa siku.Kushoto ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo,Matina Nkurlu na Mkurugenzi wa Global Publishers, Abdallah Mrisho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...