Na George Simon, Lilongwe
Ankal, nipe lau nafasi. nipate kusema na Watanzania wenzangu kuhusu mustakabali wa nchi yetu Tanzania. Thank you in advance....
NIKIWA mbali na nyumbani nimejitahidi kuwa mvumilivu lakini naona uvumilivu unanishinda. Nakufikiria nyumbani kwangu, nawafikiria ndugu zangu, nazifikiria shughuli zao, biashara zao, utalii, ufugaji, kazi za wasanii, vijana waliojipatia ajira ya kusindikiza wageni kwenye vivutio (tour guides) na wengine wengi.
Kwa kweli naona giza nene mbele yangu. Imekuwa bahati mbaya tu kwamba sioni kama hili ninaloliwaza mimi nikiwa nje ya nchi linazungumzwa na ndugu zangu waliopo nyumbani hasa vijana ambao ndio tegemeo la taifa na ndio nguvu kazi inayotegemewa.
Naandika haya nikiwa natafakari harakati za kisiasa zinazoendelea nchini mwangu hasa kwa wanasiasa waliopo upinzani ambao wengi wao ni wabunge wanaoendesha fukuto la mapambano dhidi ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Naomba niweke wazi kuwa japokuwa mimi sio mwanasiasa lakini ni mfuatiliaji mkubwa wa shughuli za wanasiasa tena kwa sababu nipo nje ya nchi hujikuta kazi hii ya kufuatilia shughuli za kisiasa zinazoendelea nyumbani inanigharimu muda mwingi na fedha.
Kwa hili ninaloliona kuwa ni harakati za wanasiasa wa upinzani kuendesha fukuto la mapambano dhidi ya serikali ya Rais Magufuli ambayo imejipambanua sio tu nchini Tanzania bali duniani kote kuwa imeamua kurekebisha makosa yaliyofanywa na serikali katika awamu zilizopita, linanishangaza sana.
Kusoma makala yote BOFYA HAPA
Kusoma makala yote BOFYA HAPA



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...