Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa Msikiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri wa jijini Dar es salaam wakati alipowasili msikitini hapo kushiriki katika fuatari Julai 3, 2016. Kushoto ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhaji Mussa Salum na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi wakishiriki katika swala kabla ya kufuturu kwenye Msikiti wa Khona Shia Ithna-Asheri wa jijini Dar es salaam Julai 3, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi alipozungumza katika futari iliyoandaliwa katika Msikiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri wa jijini Dar es salaam Julai 3, 2016. Wanne kushoto ni ni Mufti Mkuu wa Tanzania, Abukakary Zubery bin Ally na watano kushoto ni Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri, Azim Dewji.
Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri, Azim Dewji akizungumza katika futari iliyoandaliwa kwenye Msikiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri wa jijini Dar es salaam Julai 3, 2016. Mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Baadhi ya washiriki wa futari iliyoandaliwa kwenye Msikiti wa Khoja Shia Ithna-Asheri jijini Dar es salaam wakimsikiliza mgeni rasmi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza Julai 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...