Mkuu wa Mkoa wa Mbaye Mh. Amos Makalla amepongeza viongozi, watendaji na wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kwa kukamilisha utengenezaji wa Madawati elfu 32 (32,000) katika Halmashauri Sita za Mkoa wa Mbeya ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais kuhakikisha kila Mtoto anakaa katika Dawati. Hayo ameyasema leo wakati wa hafla ya kukabidhi mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Songwe.
Mkuu wa mkoa wa mbeya Amos Makalla akipokea salamu kutoka kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, George Jackson Mbijima Katika hafra ya kukabidhi mwenge mkoani songwe.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla Sanjari na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, George Jackson Mbijima wakiwaongoza baadhi ya Wanajeshi na Wananchi wa Mkoa wa Songwe katika Hafra ya kuukabidhi Mwenge wa Uhuru Mkoani Songwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...