Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki na mameneja wa vyuo na shule binafsi Tanzania (TAMONGSCO) Mrinde Mzanva akiongea na wamiliki na mameneja wa vyuo na shule binafsi kanda ya Dodoma na kuishukuru Mamlaka ya Elimu Tanzania kwa kuwa tayari kusaidia chama hicho katika kuhakikisha wanachangia katika ukuaji wa sekta ya elimu nchini.Kushoto Mwekahazina Taifa wa Chama hicho Bw.Yona Mapenzi na Kulia Mwenyekiti wa Chama hicho kanda ya Dodoma Bw.Revocatus Majuto
Meneja Mawasilano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bi. Sylvia Lupembe akiongea na wanachama wa Chama cha Wamiliki na Mameneja wa Vyuo na Shule Binafsi Tanzania (TAMONGSCO) katika kanda ya Dodoma na kuwataka kuendelea kuwa karibu na Mamlaka hiyo hasa pale wanapohitaji misaada na mikopo kwa ajili ya kuendeleza shule na vyuo vyao ili kuweza kusaidiana na serikali katika kukuza na kuendeleza sekta ya elimu nchini.
Meneja Mawasilano na Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bi. Sylvia Lupembe akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa Chama cha Wamiliki na Mameneja wa Vyuo na Shule Binafsi Tanzania (TAMONGSCO) kanda ya Dodoma Leo Mjini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...