Viongozi wapya wa TUGHE tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya uchaguzi.

ABBAS Rweyumamu amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (TUGHE), tawi la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

Katika uchaguzi huo uliosimamiwa na Katibu Mkuu wa TUGHE mkoa wa Dar es Salaam, Gaudence Kadyango , ulishirikisha wanachama 36 kutoka idara mbalimbali, ambapo Rweyumamu alishinda kwa kura 18, akimshinda Teobald Benignus aliyepata kura 17.

Nafasi ya Katibu Mkuu ilikwenda kwa Thawabu Njeni aliyemshinda Simon Mbogo baada ya kutumika utaratibu wa kura ya veto, kwa majina yao kuandika kwenye karatasi na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa JNIA, Efatha Lyimo kuokota lililoandikwa jina lake, baada ya kufungana mara mbili na mpinzani wake kwa kura 18.

Wajumbe wote nane waliogombea na kupitishwa bila kupingwa ni Tobald Benignus, Simon Mbogo, Rehema Ambali, Hussein Msuya, Sadik Milulu, Philbery Lyimo, Mwanaheri Omari na Adventina Rugimbirwa. 

Uwakilishi wa vijana umekwenda kwa Mwanaisha Athuman aliyepata kura 20, na kumshinda Lydia Mwenisongole aliyepata kura 10; huku nafasi ya uwakilishi wa walemavu umekwenda kwa Baltazar Kidiga.

Kwa upande wa kamati ya wanawake Uenyekiti umekwenda kwa Sumayi Ngasani, wakati Mweka hazina kachaguliwa Stumai Mbato na mjumbe ni Mastidia Ndyomlwango.

 Waliochaguliwa kuwa wajumbe wa kamati ya wanawake ni Justa Emmanuel na Joyce Chisongela.

Naye mwakilishi wa DNIA, Lyimo mbali na kuupongeza uongozi huo, ameutaka kutenda haki na wasiende kuwa mgombanishi kati ya muajiri na muajiriwa, ila walete ushirikiano baina ya pande hizo mbili.

Lyimo pia aliwataka viongozi hao kuweka wazi mapato na matumizi kwa wanachama wake, ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima, na pia waangalie sababu za wanachama wengi kujiengua kwenye chama hicho.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA SHERIA NA MAHUSIANO TAA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...