Mabasi yakifukuzana mlima wa Kitonga kuelekea Iringa. Wananchi wengi waliohojiwa na Globu ya Jamii wamependekeza kuwepo na adhabu ya kifungo gerezani moja kwa moja bila kuwepo na faini ya aina yoyote kwa dereva wa mabasi ya abiria na magari mengine kwa kosa lolote lenye kuhatarisha maisha ya watu. Wananchi hao wametolea mfano njia za mabasi ya mwendo kasi jijini Dar es salaam ambapo wananchi hivi sasa wanaziheshimu njia za mabasi hayo baada ya watu kadhaa kupewa adhabu ya vifungo gerezani bila faini.
Alama barabarani hapo zinamaanisha HAKUNA KUPITA KABISA lakini dereva wa basi anapuyanga tu, tena kwenye kona kona za mlima Kitonga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...