Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeshirikiana na  UMOJA SWITCH ATMS katika kuwawezesha wateja wake wa Airtel Money kufurahia huduma za kifedha na kutoa pesa kwenye mashine za ATM za UMOJA SWITCH nchi nzima bila kuwa na kadi ya ATM. 
Ushirikiano huu mpya utasaidia kurahisisha huduma za kifedha kwa watanzania na kuwawezesha kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa ufanisi zaidi, wateja wa Airtel sasa wanaweza kupata huduma za kifedha wakati wowote masaa 24 siku 7 za wiki kupitia mashine za UMOJA SWITCH ATMs zilizoendea nchi nzima
ushirikiano huu pia utasaidia  katika kutanua wigo wa mawakala wa Airtel Money ambapo wateja wa Airtel hawatakuwa na haja ya kufungua akaunti ya benki wala kuwa na ya kadi ya ATM ili kupata huduma hii, kwa kupitia mashine za UMOJA SWITCH ATMs mteja ataweza kufanya muamala kutoka kwenye simu yake ya mkononi na maramoja kutoa pesa zake kwenye mashine ya ATM kwa gharama nafuu. Kiwango kidogo kitatozwa kama tozo kulingana na kiasi cha pesa ambacho mteja atatoa.

 Meneja Kitengo cha Airtel Money, Moses Alphonce akitoa pesa katika mashine za ATM za UMOJA SWITCH mara baada ya kufanya muamala wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya Airtel na UMOJA SWITCH  utakaowawezesha wateja wa Airtel Money kutoa pesa kutoka kwenye akaunti zao za Airtel Money katika ATMS za Umoja Switch nchi nzima. Akishuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa UMOJA SWITCH, Bwana Danford Mbillinyi
 Meneja Kitengo cha Airtel Money, Moses Alphonce pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa UMOJA SWITCH, Bwana Danford Mbillinyi wakipongezana mara baada ya kuzindua ushirikiano kati ya Airtel na UMOJA SWITCH utakaowawezesha wateja wa Airtel Money kutoa pesa  katika kutoka kwenye akaunti zao za Airtel Money katika ATMS za Umoja Switch nchi nzima.

Meneja Kitengo cha Airtel Money, Moses Alphonce akitoa pesa kwenye ATM katika mashine za ATM za UMOJA SWITCH mara baada ya kufanya muamala wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya Airtel na UMOJA SWITCH  utakaowawezesha wateja wa Airtel Money kutoa pesa  kutoka kwenye akaunti zao za Airtel Money katika ATMS za Umoja Switch nchi nzima. Akishuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa UMOJA SWITCH, Bwana Danford Mbillinyi. Taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...