Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, imempata Meya mpya na Naibu wake baada ya kufanyika kwa uchaguzi wa madiwani wake Desemba 17, 2015. Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeweza kuibuka na ushindi wa nafasi zote mbili.
Manispaa hiyo imefanya uchaguzi ikiwa ni baada ya kuundwa kwa wilaya mpya mbili ndani ya Jiji la Dar es salaam, ambazo ni Ubungo na Kigambo na kufanya jiji la Dar es Salaam kuwa na Manispaa tano zikiwepo zile za awali za Ilala, Temeke na Kinondoni.
Haya ndio matokeo ya kura hizo.
Matokeo ya Meya
Kura zilizopigwa- 15
Kura iliyoharibika- 1
Maabadi Suleiman Hoja (CCM-Pembamnazi)- 9
Celestine Maufi (CDM-Mjimwema)- 5
Matokeo ya Naibu Meya
Kura zilizopigwa- 15
Amin Sambo (CCM-Kibada)- 10
Ernest Mafimbo (CUF-Tungi)- 5.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...