Na Biseko Lisso Ibrahim, MWUUM

JUKUMU kubwa la Serikali ni kuwa na miundombinu imara ili miundombinu hiyo itumike kurahisisha huduma mbalimbali zinazotolewa na hatimaye kuinua pato kwa Taifa na wananchi kwa ujumla, hii inaweza kutekelezwa kwa kutumia fedha za ndani ambazo zinatokana na kodi zinazokusanywa lakini pia kwa kupata fedha kutoka kwa wahisani wa maendeleo.

Kwa mwaka huu wa fedha 2016/2017 kwenye eneo la Miundombinu inayojumuisha barabara, reli, nyumba, bandari, viwanja vya ndege, mawasiliano. Serikali imetenga zaidi ya shilingi Trilioni 2 ili kuhakikisha miundombinu inayojengwa katika maeneno mbalimbali nchini inakuwa imara na bora na ya manufaa kwa wananchi wa Tanzania.
Makala hii itajikita kwenye eneo la reli ambapo Serikali imetenga takribani shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kujenga miundombinu ya Reli ya kisasa ambayo itarahisisha usafiri wa reli hapa nchini.

Katika uboreshaji, ujenzi na ukarabati Serikali inategemea kujenga reli mpya ya kisasa ambayo inajulikana kama Standard Gauge pamoja na mpango huo kabambe pia kuna mipango mbalimbali ya kupunguza msongamano wa magari barabara kwa kuhakikisha jiji la Dar es Salaam linakuwa na treni zaidi ya moja ili iwe inawatoa wananchi kutoka sehemu kwenda sehemu nyingine na kurahisisha shughuli zao za kila siku.

Mpaka sasa jitihada zilizofanyika katika kutekeleza hilo ni kuanzisha treni ya kutoka Stesheni hadi Ubungo maarufu kama treni ya Mwakyembe, treni ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wanakaa maeneo ya kuanzia stesheni mpaka ubungo.
Wiki ya kwanza ya mwezi wa Agosti, 2016, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alizindua treni nyingine yenye mabehewa 16 inayofanya safari zake kutoka Stesheni Dar es Salaam mpaka Pugu ikiwa ni utekelezaji wa ahadi za Serikali katika msongamano wa magari barabarani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...