Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
WAFANYABIASHARA ndogo ndogo wa Kariakoo wametakiwa kuuza bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani ili kukuza uchumi wa viwanda. Hayo ameyasema leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipokutana na wafanyabiashara wandogo wandogo wa Kariakoo, amesema bidhaa zinazozalishwa katika viwanda vya ndani zikipata soko nchi itapata mapato pamoja na kukuza uchumi wa nchi yetu.
Amesema serikali iko pamoja na wamachinga kuhakikisha wanafanya biashara kwa mujibu wa sheria kwa kuuza vitu vyenye ubora na wakibaini kuwepo kwa vitu ambavyo vinahatarisha maisha ya watanzania watachukuliwa hatua mara moja.
Makonda amesema ni marufuku wageni kutoka nje ya nchi kufanyabiashara ya umachinga katika jiji la Dar es Salaam wao wanatakiwa kuleta utaalam tu. Aidha amewaasa wamachinga kuwafichua wale ambao wanaweka rebo katika bidhaa wakati hawazalishi wenyewe.Makonda amesema katika maeneo ambayo wanafanyia kazi wamachinga kufuata sheria na kanuni zilizowekwa bila kuharibu utaratibu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akizungumza nawafanyabiashara ndogo ndogo marufu kama Machinga mtaa wa Kongo na kusikiliza kero zao leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akizungumza wafanyabiashara wa soko kuu la Kariakoo nakusikiliza kero zao leo jijiji Dar es Salaam.
Ofisa Tawala wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akifafanua jambo katika mkutano waMachinga mtaa wa Kongo leo jijiji Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...