Waheshimiwa Viongozi,
Karibuni sana kwenye Maonesho ya Kwanza ya Viwanda vya Tanzania yatakayofanyika katika Uwanja wa Maonesho ya Biashara wa Mwl. J.K. Nyerere, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam kuanzia tarehe 7 - 11 Desemba 2016.
Mpaka sasa kuna viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vya Tanzania vipatavyo 400 ambavyo vimethibitisha kushiriki.
Tunawaomba Viongozi wote ambao wangependa kutembelea Maonesho haya, watufahamishe kupitia: Simu +255 22 2850238, +255 714 077 649, barua pepe: info@tantrade.or.tz ili tuwaandalie Protokali waweze kutembelea washiriki ambao wangependa kuwatembelea. Karibuni sana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...