Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Shirikisho la soka nchini TFF limesema kuwa ligi kuu ya Vodacom haitasimama kwa ajili ya kupisha kombe la mapindzu bali vyote vitakwenda sambamba.

Hayo yamesemwa na afisa mtendaji mkuu wa bodi ya ligi nchini, Boniface Wambura alipokuwa akizungumza na kituo kimoja cha televisheni juu ya muingilio wa ligi hiyo na ligi kuu ya Vodacom.

“lazima watu watambue kuwa TFF katika hili tumejipanga kwa kushirikiana na wenzetu shirikisho la soko visiwani Zanzibar(ZFA) kwa kutengeneza ratiba ambayo aiwezi kuathiri wala kupelekea kusimamishwa kwa ligi kuu bara ambayo inaendelea hivi sasa”amesema Wambura.

Amesema kuwa katika kuzingatia hilo timu zinazoshiriki ligi ya mapinduzi kutoka bara ni tatu hivyo zote zimeweza kutengewa muda wa kucheza mapinduzi kisha kurejea kucheza michezo ya ligi kama ratiba inavyo hitaji .

Ameweka wazi kutokana na ratiba ya mapinduzi timu zote zinazoshiriki ligi kuu bara ni lazima zitafuata makubaliano ya kucheza michezo mingine visiwani kisha kurejea kucheza michezo ya ligi kama ilivyopangwa.

Wambura aliwatoa hofu wapenzi wa ligi kuu ya Vodacom kuwa na amani kwa ligi itaendelea kama ilivyopangwa nchi nzima.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...