NA K-VIS
BLOG, Iringa
MRADI wa
umeme wa Backbone wa ujenzi wa njia kuu ya umeme ya msongo wa Kilovolti 400 ya
urefu wa Kilomita 670 kutoka Iringa hadi Shinyanga kupitia mikoa ya Dodoma na
Singida, umekamilika kwa asilimia 100, Meneja wa Mradi huo, Mhandisi
Khalid Reuben James amewaambia wahariri wa vyombo vya habari mjini Iringa leo
Desemba 19, 2016.
Pia mradi
huo unaohusisha kukamilika kwa upanuzi wa vituo vine vya kupoza na kusambaza
umeme kwenye mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga utawezesha kuvipatia
umeme vijiji takriban 121, vinavyopitiwa na mradi huo, alisema Mhandisi James.
“Mradi huu
ni wa muhimu sana kwenye gridi ya taifa kwa sababu utaongeza uwezo wa
kusafirisha umeme kutoka kanda ya Kusini Magharibi, ambako kuna vyanzo vingi
vya umeme na kupeleka Kanda ya Kaskazini Magharibi ambako kuna shughuli nyingi
za kiuchumi ikiwemo migodi ya madini.” Alifafanua Mhandisi James.
Kwa mujibu
wa Mhandisi huyo, mradi huo ulianza mwaka 2013, na ulikadiriwa kugharimu kiasi
cha Dola za Kimarekani Milioni 470, ambazo zimetolewa na Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, na wafadhili wakiwemo, Benki ya Dunia, dola za
Kimarekani, milioni 150, Benki ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB), na
Shirika la Maendeleo la Kijapani, (JICA), Dola za Kimarekani milioni 129.7,
Benki ya Uwekezaji ya nchi za Jumuiya ya Ulaya, (EIB), Dola za Kimarekani
milioni, 134.5, Shirika la Kiuchumi la Maendeleo ya Korea ya Kusini, (EDCF),
Dola za Kimarekani milioni 36.416, na Serikali ya Norway, Sweden na Tanzania,
kupitia kwa wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dola za Kimarekani milioni 33.4.
“ Ndugu
zangu, mradi huu unatoa hakikisho kwa serikali kuwa mipango yake ya kujenga
uchumi wa viwanda unawekana pasina shaka, kwani mradi huo mkubwa, utawezesha
sasa, kuwapatia wateja umeme ulio bora na wa uhakika,” alsiema.
Waandishi wa
habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, wako kwenye ziara ya
kutembelea mradi huo ambao unatarajiwa kuzinduliwa rasmi mapema mwezi Januari,
2017.
Meneja wa mradi mkubwa wa umeme wa Backbone, Mhandisi Khalid Reuben James, akitoa maelezo kwa wahariri (jawapo pichani), walipotebelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Tagamenda kilichoko nje kidogo ya mji wa Iringa, wakati wa ziara ya wahariri kukagua ujenzi wa mradi wa Backbone unaotoka mkoani Iringa hadi Shinyanga kupitia mikoa ya Dodoma na Singida, Desemba 19, 2016
Wahariri wakitembelea mitambo ya umeme kituo cha Tagamenda
Mhandisi huyu wa Tanesco, akitumia ramani ya mradi huo kuwaelimisha wahariri ukubwa wa mradi huo
Wahariri wakiangalia nguzo zinazobeba nyaya (conductors), za mradi wa Backbone, kwenye kituo cha Tagamenda.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...