
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa kawanza kulia), kuhusu maendeleo ya miradi ya ujenzi wa barabara nchini inayotekelezwa na shirika hilo. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mkuu (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akifurahia jambo na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa kawanza kulia), walipokutana jjijini Dar es salaam leo. Kushoto kwa Makamu wa Rais wa JICA ni Mwakilishi Mkuu wa JICA Tanzania Bw. Toshio Nagase.

Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa walipokutana jijini Dar es salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kulia), na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa tatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wao mara baada ya kujadili mikakati ya kuboresha miundombinu nchini.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...