Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo (Kulia), akifafanua jambo kwa Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na
Mazingira wa Zanzibar, Mhe. Salama Aboud Talib, wakati wa mazungumzo yao kuhusu
ushirikiano baina ya Wizara hizo mbili hususan katika sekta ya nishati. Waziri
Talib alimtembelea Waziri Muhongo ofisini kwake jijini Dar es Salaam
![]() |
| Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira wa Zanzibar, Mhe. Salama Aboud Talib, mara baada ya mazungumzo kuhusu ushirikiano baina ya Wizara hizo mbili hususan katika sekta ya nishati yaliyofanyika Ofisini kwa Waziri Muhongo jijini Dar es Salaam, hivi karibuni. |
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia) akiwa katika picha ya
pamoja na Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Kochanke baada ya mazungumzo
yao. Balozi Kochanke alimtembelea Waziri Muhongo hivi
karibuni Ofisini kwake jijini Dar es Salaam na kuzungumzia ushirikiano baina ya
nchi hizo mbili hususan katika sekta ya nishati.
![]() |
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia), akitazama kabrasha
alilopatiwa na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke (katikati),
linaloonesha maeneo ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili hususan katika
sekta ya nishati. Kushoto ni Ofisa kutoka Ubalozi huo, Julia Hannig. Balozi
Kochanke alimtembelea Waziri Muhongo hivi karibuni ofisini kwake jijini Dar es
Salaam.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...